Search lyrics

Typing something do you want to search. Exam: Artist, Song, Album,Writer, Release Year...
if you want to find exactly, Please input keywords with double-quote or using multi keywords. Exam: "Keyword 1" "Keyword 2"

Singles


Artist: Kidum
Total songs: 2
Year:

List songs in album

  1. Nitafanya
  2. Mapenzi

Nitafanya Lyrics - Singles - Kidum

Verse 1(Kidum) 

Ikiwa umeamua kunitoroka 

ikiwa unahisi hujiskii nami tena 

na mbona imekuwa ngumu kunidokeza 

naona ni bora nilie leo, badala ya kesho 

kupenda, usipende 

ni kama kujitia kitanzi 

nitachimba na sururu 

kwa ardhi nikitafuta penzi lako 

ni heri nipigwe fimbo kwa mwili 

sababu ntajikuna ama ntajikanda na maji moto 

maumivu ya penzi, mtu hajikuni 

wala hajikandi na maji 

na hakuna upasuaji 

 

Chorus 

kama 

kuna kosa nimewahi fanya(nielezee) 

kama 

kuna jinsi tunaweza leta(mpaka niishi) 

na kama 

kuna kitendo linaweza tendwa(nielezee) 

 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

 

Verse 2(Lady Jay Dee) 

kweli hukumbuki ulioyafanya 

ni kweli unakumbuka tulikotoka 

sisemi habari zozote za kusikia 

bali kwa ushahidi niliouona 

msamaha mara ngapi 

umeshaomba na bado 

chenye makosa mangapi 

niliyoyafumbia macho 

mpaka leo nahisi kufika kikomo 

maumivu yanazidi 

ndani ya moyo 

sitaki kwenda mbali kwani uko moyoni 

nikusamehe mimi mara ngapi wee 

nielezee mpenzi mara ngapi 

 

Chorus 

unataka nikusamehe mara ngapi(usihesabu) 

ungependa nikuvumilie mara ngapi(hii ni ya mwisho) 

je wewe nikulilie mara ngapi(vumilia) 

 

sitoweza(utaweza wee) 

nimechoka(usichoke) 

nimeshindwa(usishindwe) 

naondoka(usiondoke) 

 

sitoweza(utaweza yee) 

nimechoka 

nimeshindwa(usishindwe) 

naondoka(usishindwe) 

 

Verse 3 

ukihesabu mara ngapi umenisamehe 

ni kama kuhesabu 

ni mara ngapi mtoto kaharibu nappy 

usichoke 

usiondoke 

usilie 

niko hapa kukulinda 

 

Chorus 

kama 

kuna kosa nimewahi fanya(nielezee) 

kama 

kuna jinsi tunaweza leta(mpaka niishi) 

na kama 

kuna kitendo lingeweza tendwa(nielezee) 

 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

nitafanya(fanya) 

nitatenda(tenda) 

 

unataka nikusamehe mara ngapi(usihesabu) 

ungependa nikuvumilie mara ngapi(hii ni ya mwisho) 

je wewe nikulilie mara ngapi(vumilia) 

 

sitoweza(utaweza wee) 

nimechoka(usichoke) 

nimeshindwa(usishindwe) 

naondoka(usiondoke) 

 

sitoweza(utaweza yee) 

nimechoka 

nimeshindwa(usishindwe) 

naondoka(usishindwe)